test

Jumatano, 25 Januari 2017

Makala: Jinsi ya Kukinga Kvuli Chako Kisionekane na Wachawi


IMESIMULIWA  NA  DOKTA. MUNGWA  KABILI….0744  000  473.
Wachawi  wana  uwezo  wa  kumtia  mtu  nuksi na mikosi mbalimbali.
Nuksi  na  mikosi  hiyo  inaweza  kuja  katika  sura  ya  magonjwa  na maradhi sugu  yasiyopona kama  vile kisukari, ukimwi, ugumba,  mimba kuchoropoka, kifafa  nakadhalika.
 Kufukuzwa  kazi, matatizo  katika ndoa,  ajali, umasikini, vifo  na  misiba  mfululizo, kuchukiwa  na  watu  nakadhalika.

Zipo  njia  mbalimbali  wanazo  tumia  wachawi  katika  kuwatia  watu  nuksi na mikosi, Katika  makala  ya  leo, nitaelezea  njia  moja  wapo  kama  ifuatavyo:
Katika  njia  hii, wachawi  wakitaka  kumtia  mtu  mikosi, hufanya  mambo  yafuatayo :

i.  Wanachukua  hela  ambayo  haitumiki
ii. Wanachukua   mavi ya  mbwa  mweusi ambayo  ameyanya  usiku wa manane
iii.Wanachukua  mkaa ulio kwisha  tumika, ambao  umetumika  mahali  ambapo  watu  hawalali  kama vile  kilioni  au  kwenye  baa  na migawaha  inayo  kesha lakini  mara  nyingi, huchukua  mkaa  wa  kilioni.
iv.Wanachukua  mavi   ya  ndege  anaitwa   Mumbi. Huyu ndege  aitwae  Mumbi  anapatikana  porini. Anafanana  sana  na  bata  na  ana  puyanga  la rangi  nyekundu.
v. Wanachukua  shahidi   la  kaburini  pamoja  na  ndumba  zingine  za  kichawi
vi. Wanachukua  kitu   chochote  cha  mtu  aliye  kusudiwa  kutiwa mikosi  kama  vile  jina  lake, picha  yake, mchanga  alipokanyagia, mate, kucha, au chochote  kile.
Baada  ya  hapo, mchawi  huyo  atakwenda  kaburini  usiku  wa  manane  na  kuvizika  vitu  vyote  nilivyo  vieleza  hapo  juu, huku  akisema  maneno  ya  kichawi. Basi  mtu  aliye  kusudiwa  na  uchawi  huu, kama  hana  kinga, ata andamwa  na  mikosi mikubwa  na  mizito  katika  maisha  yake  yote.

JINSI  YA  KUJIKINGA  DHIDI  YA  UCHAWI  HUU
Kujikinga  na  uchawi  huu  inabidi ufanyiwe  zindiko ama  upate  kinga maalumu  ya  kuficha  kivuli  chako. Hii  itawafanya  wachawi  washindwe  kukuona  katika  rada  zao  za  kichawi, na  wachawi  huwa  hawawezi  kumloga  mtu  ambae  haonekani  katika  rada  zao, kwa  sababu  wanawakuwa  hawajui  nguvu  zake  ziko  wapi wala  silaha  zao  haziwezi  kumshambulia mtu  ambae  haonekani  kwenye rada zao. 
Ukiwa  na  kinga  hii, hakuna  uchawi  wa  aina  yoyote  ile  unao weza  kufanyika  juu  yako, iwe  ni uchawi  wa  kukusababishia  madhara, au  uchawi  wa  mahaba  kukufunga  kimapenzi.
JINSI  YA  KUFICHA  KIVULI  CHAKO  KISIONEKANE  NA  WACHAWI
Kuficha  kivuli  chako  kisonekane  na  wachawi, fanya  kama  ifuatavyo

i.  Chukua  nywele  za  saluni
ii.  Chukua  mzizi  wa  mti  ulio  katisha  njia
iii. Chukua  tawi  la  mti  unaitwa  Ututukanga. Huu  mti  wa  Ututukanga  unapatikana  porini na baharini  na  huwa  linaonekana  shina  lake  na  matawi  yake  tu, lakini  mzizi  wake  huwa  hauonekani.
iv. Unachukua  mti   unaitwa  Msonihya
v.  Unasaga  pamoja  na  mti  unaitwa  mwavi.
vi. Baada  ya  hapo  unachukua  kuku  mweusi, unamfunga  kwenye kitambaa  cheusi  bila  kumchinja, unachukua  chungu  cheusi, unamuunguza  mpaka  anakuwa  mkaa, halafu  unamsaga  pamoja  na  miti  iliyo  tajwa  hapo  juu, unachanganya  na  mafuta  ya  simba.
vii. Unachukua  buja ama  dulya  la  ugali  wa  kilioni
viii.Unachukua kamba  ya  kitanda  alicho  lalia  maiti, au kama  maiti  ipo  kwenye  nyumba  ya  nyasi, unachomoa  nyasi  wakati  maiti  imo  ndani.
ix. Unachimba  mzizi  wa  mti  unaitwa  mputika  bila  kivuli chako  kugusa mti..
x.  Unaunguza  vyote  kwa  pamoja  ukiwa  na  kaniki  nyeusi  bila  kuvaa  nguo  yoyote  usiku wa  manane
xi. Unaipika  njia  panda pamoja na  mafuta  ya usiku.
Baada  ya  hapo, mtu  atachanjiwa  au kujichanja mwenyewe na kuoga au  kuogeshwa dawa hiyo.
Basi wachawi  watakuwa  wakijaribu  kutaka  kukutupia  uchawi, wanakuwa  hawakauoni  kwenye  rada  zao za  kichawi.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx