Waziri
wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tamisemi
Mhe. George Simbachawene ameitikia mara moja agizo lililotolewa na Rais
Dkt John Pombe Magufuli la kusitisha zoezi la kuwaondoa machinga maeneo
yasiyo rasmi
Mhe.
Simbachawene, ameitikia agizo hilo kwa kuwataka wakuu wa wilaya pamoja
na halmashauri zote nchini kuangalia ufumbuzi na utaratibu mzuri wa
kuwashirikisha wajasiriamali hao ili kupata ufumbuzi ulioshirikisha
kuliko utaratibu wa sasa wakuwafukuza bila kusikiliza madai yao.
Mhe.
Simbachawene amesema, Rais Magufuli anatambua mchango mkubwa na kazi
nzuri inayofanywa na wakuu wa wilaya katika kuleta maendeleo hivyo
kuweka maeneo sahihi kwaajili ya wafanyabiashara wadogo kutaleta maana
kubwa ya uwajibikaji.
“Kwa
kuanzia ni vema yakatengwa maeneo ya katikati ya mji yenye wateja wa
bidhaa zinazouzwa, kwa kuangalia uwezekano wa kufunga mtaa japo mmoja
ili utumike kwa kazi za kimachinga,” alisema jana Simbachawene wakati akiongea na waandishi wa habari.
Alisema usumbufu unaojitokeza maeneo mbalimbali unasababisha wananchi kupoteza mitaji yao ambayo wengine wamekopa kwenye vikundi vya vicoba na hivyo kuhatarisha mustakabali wa maisha yao na familia zao.
Alisema usumbufu unaojitokeza maeneo mbalimbali unasababisha wananchi kupoteza mitaji yao ambayo wengine wamekopa kwenye vikundi vya vicoba na hivyo kuhatarisha mustakabali wa maisha yao na familia zao.
Hivi
karibuni waziri huyu alitoa agizo kwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya
nchi nzima kuhakikisha wanawaondoa wafanyabiashara hao katika maeneo
yasiyo rasmi kwa sababu wanaleta usumbufu na uchafu, agizo ambalo lilianza kutekelezwa mara moja katika maeneo mbalimbali ikiwemo Mwanza na Dar es Salaam.