test

Alhamisi, 8 Desemba 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 49 & 50 (Mwisho)


Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA  
“Tumekupata”
Alipokea jibu mmoja kutoka, makao makuu. Wakaendelea kujibu mashambulizi ya watu hao ambao wamewavamia na hawakujua niwatu wangapi. Hali katika eneo la mto ikazidi kuwa mbaya zaidi milio ya bunduki, ilizidi kurindima kila kona.
“Helcoptar…..!!!”
Anna alishangaa baada ya kuona helcoptar zipatazo sita za jeshi la marekani zikifika katika eneo hilo, huku wajeshi wengi wakishuka kwenye helcoptar hizo zilizopo hewani, kwa kutumia kamba ndefu hadi chini.
‘Tunakufa leo’
Halima alijisemea kimoyo moyo huku akiendelea kuftyatua risasi nyingi kuelekea walipo wanajeshi hao.

ENDELEA
“Sister nguvu yetu imesha anza kuwa ndogo tunafanyaje”
Jamaa mmoja alizungumza huku akibadili magazine ya mwisho katika bunduki yake na endapo risasi zitakwisha kwenye magazine hiyo, basi hatokuwa na msaada wowote.
“Endelea kupambana hatuwezi kurudi nyuma”

Fetty alizungumza huku akizendelea kufyatua risasi kuelekea walipo wanajeshi hao
“Fetty eheee omba msaada kwa mkuu, lasivyo tutakufa humu”
Halima alilalamika kama kawaida yake, Fetty kutazama idadi ya wanajeshi wanao shuka kwenye helecoptar hizo kubwa za kijeshi, ikambidi awasilianen na bwana Rusev.
“Muheshimiwa wanajeshi wa Marekani wametuvamia”
“Endeleni kupambana”
“Sawa muheshimiwa ila tunahitaji msaada wa vijana wengine”

“Msaada….. Masaada wa nini pambaneni”
Majibu ya bwana Rusev, yakamtia hasira Fetty aliye jibanza kwenye mti huku akisikilizia jinsi risasi hizo zinavyo  zidi kupigwa kwenye sehemu walipo.
“Muheshimiwa nakuheshimu, ila narudia tena nahitaji msaada wako”
“Kama hamjampata Agnes basi, hakuna cha msaada wowote kutoka kwangu”
Mawasiliano yakakatwa, Fetry akabaki aking’ata meno yake kwa hasira. Kumbukumbu ya tukio hili likamrudisha miaka ya nyuma, jinsi siku wanajeshi wa Tanzania walivyo vamia kwenye kambi yao, na kuwashambulia sana kisha wakaingia mikononi mwao wanajeshi hao, hapo ndipo ulipo kuwa mwisho wa maisha yao ya furaha na amani na wakajikuta wakiwa wanaishi kama wakimbizi na kukubali kufanya kazi na watu ambao ni magaidi wa kidunia, ili mradi waweze kuendelea kuishi kwenye maisha haya.

Fetty akiwa katika mawazo hayo, akamshuhudia kijana mmoja wa bwana Rusev akianguka chini, baada ya kupigwa risasi ya kichwa, akiwa anashangaa tukio hilo, kijana mwengine akajitokea kwa hasira kwenye mti alio kuwa amejificha huku akiwa na bastola mbili mkononi mwake, akifyatua risasi zisizo na idadi, ila alicho weza kukutana nacho, ni mvua ya risasi zizizo toka kwenye jeshi lilio wazidi nguvu.
“Fetty amesemaje”
Halima alizungumza huku machozi yakimlenga lenga.
“Mmmmmm…….”
“Amesemaje mkuuuuuu…..”
“Hana msaada na sisi, tupambane kama kufa tufe ila si kukamatwa”

“Mungu weeeee, nini sasa hichi”
Halima alizungumza huku machozi yakimwagika, akachomo magazine kwenye bunduki yake na kukuta ikiwa na risasi chache, akajipapasa hana tena magazine. Akageuza kichwa sehemu alipo Anna, akamkuta akiendelea kufyatua risasi pasipo kuangalia wezake wapo katika hali gani. Vijana wawili wa bwana Rusev walio bakia, wanazidi kuyapigania maisha yao kwani ni heri kufa kuliko kukamatwa na jeshi hilo.
“Nakupenda Anna, Fetty”
Halima alizungumza kwa sauti ya unyonge, akairudishia Magazine yake kwenye bunduki, akapiga goti mmoja chini, akawatazama jinsi wanajeshi wa wanavyo zivurumisha risasi katika eneo walipo.
“One one one bullet”(Mtu mmoja, risasi moja)
Halima alizungumza huku akiendelea kufyatatua risasi kwa kila aliye weza kumuona kwa wakati huo. Ila zilipo fika risasi kumi na mbili, bunduki yake ikagoma kutoa risasi, ikiashiria kwamba hakuna risasi nyingine ndani ya bunduki hiyo aina ya AK47, zinazo tumika sana nchini Russia.
                                                                                                 ***  
     Asubuhi na mapema, raisi Praygod akakurupuka kitandani, akaka kitako huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi sana. Rahabu taratibu akajinyanyua na kumtazama jinsi anavyo tokwa na jasho jingi mwilini.
“Una tatizo gani mume wangu?”
“Naota mandoto mabaya mabaya tu”
“Ohoo pole mume wangu”

Rahab alizungumza huku akimkumbatia raisi Praygod, taratibu akaanza kumpapasa kifuani mwake, hisia za mapenzi zikaanza kuusisimua mwili wa raisi Praygod, taratibu akajikuta akianza kumnyonya mke wake mdomo, baada ya muda wakajikuta wakizama kwenye dimbwi zito la kupena haki ya wanandoa.
Baada ya kumaliza wakaingia bafuni kuoga, Rahab akamuandalia mume wake nguo za kuvaa kwenye kikao anacho kwenda kukifanya na wakuu wote wa kitengo cha usalama wa taifa.
“Leo nitapendeza sana mke wangu”
“Kwa nini?”
“Umenichagulia nguo wewe”
“Ahaaa si kawaida”
“Sawa ila utapendeza sana, siku zote nimezoea kujichagulia nguo mwenyewe”

“Ila si una wafanyakazi wenye jukumu hili?”
“Ndio ila mke wangu upo kwa nini nichaguliwe na mfanyakazi”
“Hapa utakuwa poa sana”
Rahab alizungumza baada ya kumfunga tai raisi Praygod, akampiga busu la mdomoni
“Twende tukapate kifungua kinywa pamoja”
Wakatoka na kwenda kwenye sebla yao, ambapo wakakuta chakula tayari kimesha andaliwa na kukaguliwa na daktari maalumu anaye weza kukagua chakula cha raisi kabla hajakila. Wakapata chakula baada ya kumaliza akaomba kuweza kuitiwa wafanyakazi wote wa ikulu, ikawa kama alivyo agiza.
“Nimewaita hapa kutokana nahitaji kuwatambulisha mama yenu, so mukimuona huko nje misije mukamdharau.”
“Muheshimuni kama munavyo niheshimu mimi, mpendeni kama munavyo nipenda mimi. Nisinge penda mtu yoyote kuweza kuona mtu ana….ana anaa mkosea adabu”
“Mumenielewa”

Ndio muheshimiwa”
Baada ya utambulisho huo, raisi Praygod akawaamuru wafanyakazi wake kuweza kuondoka, akabaki na mke wake. Akamtuma mmoja wa walinzi wake kwenda kumuita Samson kwenye chumba chake. Samson akafika katika sehemu walipo.
“Umeamkaje muheshimiwa”
Samson alisalimia kwa heshima
“Salama tu kaa”
“Madam Rahab je wewe umeakaje?”
“Nipo salama”
Kwa nguvu aliyo weza kumuwekea Samson. Rahab anamamlaka makubwa ya kuweza kumuamrisha Samson, akafanya kile alicho weza kumuambia.
“Jiandaeni kwani nitawahitaji kwenye kikao baada ya muda fulani hivi”
“Baby kwa nini sisi?”
“Nahitaji tusaidiane katika kuirudisha heshima ya nchi, pia kesho tutakwenda kwenye misiba ya wanajeshi wali fariki walipo kuwa wakimsafirisha makamu wa raisi”
“Kwani hawakuzikwa?”

“Ndio, hawajazikwa, nimeagiza kwamba iwe siku ya maombolezi kwani pia wale wananchi walio poteza maisha uwanja wataifa inabdidi kuzikwa kesho”
“Sawa”
Raisi Praygod akawaaga, akaongozana na walinzi wake wawili hadi chumba cha mkutano.
“Hivi umempataje pataje raisi?”
Samson alizungumza huku akiachia tabasamu pana usoni mwake
“Ni story ndefu sana, tangu tuachane pale kwenye ndege basi ikawa ndio siku ya mimi kuweza kuonana na raisi Pray”
“Ahaaa maisha haya bwana, adui yako amekuwa mume wako”
“Usiongee kwa sauti kubwa, tusije kuhisiwa vibaya. Ila kusema kweli ninampenda mume wangu”
Samson hakuwa na chakuzungumza zaidi ya kuanza kupata kifungua kinywa, Rahab akaondoka na kuelekea chumbani kwao kujiandaa na kikao ambacho mume wake alimuhitaji kuweza kufika.
                                                                                      ***
“Kila mmoja ninaamini ameyaona yaliyo jitokeza.”
“Nchi imepata fedheha mbele ya wageni, walio huzuria msiba ulio kuwa wangu pamoja na wahanga wengine. Kiongozi mkubwa wa nchi kuweza kufanya mambo ambayo yangefanywa na wagaidi ameweza kuyafanya yeye.”
“Inaonekana ni jinsi gani, kitengo chenu, kilivyo jisahau kwa asiliimia nyingi tuu kwani hadi inafikia hatua ya matukio ya ajabu kama kushambuliwa kwa wanajeshi na makamu wa raisi kutoroshwa, yote ni uzembe na inavyo onekana anamiliki kundi kubwa la vijana anao weza kuwatumia katika kuleta machafuko kwenye nchi hii.”

Raisi Praygod alizungumza kwa saut iliyo jaa msisitizo mkubwa huku akiwatazama viongozi hao wapatao kumi na mbili walio izunguka meza kubwa katika eneo hilo.
“Yote yaliyo weza kujitokeza, hayaweze kubadilika, ila tunaweza kuyafanya wananchi wakaweza kutuamini na kuishi kwa amani. Kwani inavyo onekana hali ya amni imekuwa tata kwa wananchi.”
“Hivyo basi, nitahakikisha kwamba tunafanya kazi, iliyo wafanya kila mmoja wenu kuwa katika kitengo alicho kuwepo. Hata mimi mwenyewe nitahakikisha kwamba ninafanya kazi zote zakijeshi kama ni kuua basi tuue yule anaye stahili kuuliwa.”
“Sinto kuwa na msamaha kwa mtu ambaye ukimpa nafasi moja, anakuua wewe. Kuanzia sasa nahitaji kusikia ni wapi alipo makamu wa raisi wangu, yeye na kundi lake tuweze kuwatia nguvuni kwa pamoja. Nakaribisha maoni”

Raisi  Praygod akazima maiki yake aliyo kuwa akitumia kuzungumzia. Kiongozi mmoja akanyoosha kidole na raisi Praygod akampa nafasi ya kuzungumza
“Muheshimiwa, kwanza tuombe radhi ya yale yaliyo jitokeza. Pili tumeweza kupata sehemu ambayo makamu wako amejificha na kundi lake”
“Ni hapa ndani ya nchi?”
Raisi Praygod alizungumza huku akimtumbulia macho kiongozi huyo.
“Hapana si ndani ya nchi hii, ila yupo nchini Kenya, na taarifa hizi tulizipata kwa wana usalama wa nchi ya Kenya”
“Eheee mu..mu muu mumejipangaje?”
“Tulimesha andaa taskforce kuweza kuvamia katika sehemu hiyo, huku tukishirikiana na interpol”
“Fanyeni mawasiliano na raisi wa Kenya sasa hivi nizungumze naye”
                                                                                    ***
“Kwa nini memenisaidia?”
Agnes aliuliza swali baada ya kumaliza kupata kifungua kinywa akiwa na Jackline pamoja na Monk
“Kwani inatubidi kurudi nchini kwetu kuimarisha ulinzi na si kuendelea kutumika katika vikosi vya ajabu”
“Umejuaje kama ni vikosi vya ajabu na umenifamu fahamu vipi mimi?”
Agnes aliendelea kumuuliza maswali Jackline ili kuweza kumfahamu vizuri
“Kipindi nyinyi munakuja kwenye ngome ya bwana Rusev, mimi nilikuwa ni miongoni mwa walinzi wake wakaribu. Wiki moja baada ya nyinyi kufika pale mimi nilipewa kazi ya kwenda kumuangamiza raisi wa Korea kaskazini.”

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx