test

Alhamisi, 8 Desemba 2016

Rais Magufuli awapandisha vyeo Maafisa Wakuu wawili wa JWTZ kuwa Meja Jenerali



ais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewapandisha vyeo Maafisa Wakuu wawili wa JWTZ kuwa Meja Jenerali kuanzia tarehe 03 Disemba 2016. Maafisa Wakuu hao ni;

Brigedia Jenerali George William Ingram ambaye ni Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga, na  Brigedia Jenerali Michael Wambura Isamuhyo ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Adolf Mwamunyange kwa niaba ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu anawapongeza na kuwatakia kheri katika vyeo vyao vipya.
 

Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na
Uhusiano Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   

Dar es Salaam,  Tanzania.

Kwa Mawasiliano zaidi: 0784-477638/0756-716085
R5
Brigedia Jenerali George William Ingram ambaye ni Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga
Brigedia Jenerali Michael Wambura Isamuhyo ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx