test

Jumamosi, 17 Desemba 2016

MBUNGE WA MBEYA JOSEPH MBILINYI "SUGU" APATA AJALI


Hii ni ajali nyingine ya Sugu aliyoipata Januari 10, 2015 kwenye mlima wa Kitonga baada ya gari lake breki kufeli na hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa



MBEYA: Taarifa zilizoripotiwa na kituo cha runinga cha ITV leo Desemba 17, 2016 zinasema kuwa Mbunge wa Jimbo loa Mbeya Mjini (CHADEMA), Joseph Mbilinyi amenusurika kifo katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Iyunga jijini Mbeya baada ya gari lake kufeli break na kumgonga mtoto ’15’ ambaye amefariki wakati akipelekwa hospitali.

Aidha taarifa hiyo inaeleza kuwa askari polisi wanne wamejeruhiwa baada ya kupata ajali wakati wakielekea kwenye ajali hiyo aliyopata mbunge Joseph Mbilinyi ‘Sugu’
Pia imeelezwa kuwa, Mbunge Sugu ametoka akiwa salama huku dereva wake aliyekuwa akiendesha gari hilo, Gabriel Andrew (43) anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx