test

Jumatano, 9 Novemba 2016

INASIKITISHA::SOMA KISHA CHECK VIDEO MZUNGU AKIMLAZIMISHA MWAFRIKA KUINGIA KWENYE JENEZA


Johannesburg, Africa Kusini
Hisia kali zimetolewa mitandaoni baada ya mwanamume mzungu kuonekana akimwingiza mwanamume mweusi kwenye jeneza kwa lazima huku akitishia kumchoma akiwa hai


Video iliyosambazwa mitandaoni ilionyesha tukio hilo ambalo wengi wanasema ni dhihirisho la jinsi ukandamizaji wa Waafrika weusi bado unaendelezwa nchini humo
Kwenye video hiyo ya sekunde 20, Mwanamume mweusi aliyeingizwa kwenye jeneza anasikika akilia huku mzungu anayeaminika ni mkulima akifunga jeneza hilo kwa lazima
Anasikika akimwambia "Ingia ndani... ninataka kumwaga petroli"
Mwingine ambaye haonekani lakini anaaminika ndiye aliyekuwa akinasa video hiyo anasikika akitishia kuingiza nyoka ndani ya jeneza hilo kama kijana huyo mweusi ataendelea kujaribu kujinasua
Kumekuwa na malalamiko ya Waafrika weusi kuhusu ubeberu nchini humo ambapo hivi majuzi wanafunzi wa vyuo vikuu waliandamana kutaka sanamu za kibeberu zibomolewe katika vyuo vyao
Matukio mengine ambapo waafrika weusi walilazimishwa na wazungu kunywa mikojo yao, pia yamewahi kuripotiwa.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx