test

Jumapili, 2 Oktoba 2016

VIDEO:Mashabiki wa Simba wavunja viti huku Geti la uwanja likivunjwa pia


Inasikitisha sana, na inauma sana kwanini watu hawaipendi nchi yetu.Viongozi waliona vema tuwe tunaangalia mechi tukiwa tumekaa kwenye viti, lakini kuna watu wanavunja viti namna hii, yani nakosa neno la kuwaita maana hata hilo haliwafai, huko ni kujirudisha nyuma kimaendeleo na tunajidharilisha kwani kwa utandawazi wa sasa ni kuwa Dunia yote inaona. Kifupi wamekosa akili ya kujiongeza

Simba wapewe adhabu kali na hii itasaidia mashabiki kujifunza ustaarabu wa ushabiki. Sasa kila timu ikifunga mkiwa mnangoa viti huo uwanja utadumu kweli?Tuwe na uchungu na mali ya umma.
Kwa upande mwingine mashabiki walivunja geti la uwanja huo upande wa chuo cha Duce na kusababisha uharibifu mkubwa baada ya polisi kufanya jitihada za kuwatuliza kushindikana.

Tazama comments mbali mbali hapa chini kisha tazama video
Issa Katumbi 
yanga ni wanawake kweli Dada zenu wacheze rede na nyie mcheze rede basi vaeni madera ili mcheze vzuri
Emmanuel Mike 
mbona mkavunja viti?
Ally Abdallah Manditi 
Naomba jibu la swali langu jamani: Kwa uharibifu huu wa viti hivi, wewe unaona ni nani anapaswa kuwajibika kwa lawama au malipoo?! a.) Mwamuzi wa kati (Refa) b.) Tambwe c.) Mwamuzi wa upande wa kulia d.) Mwamuzi wa upande wa kushoto e.) Hakuna jibu sahihi
AD MLAY 
SIMBA SC
Emmanuel Mike 
marekebisho ya mfumo. kila tiketi iingizwe na namba ya Simu ya muhusika ikibidi hata ID YAKE tuweze kuwatrace wote. pili kwa sasa CLUB ya SIMBA iwajibike
Mohd Ali 
jamani bora mplek malalamiko sehemu husik kuliko kuharibu uwanja
ee katabi 
waamuzi wanapaswa kuwa makini na kazi zao ,mapungufu yao yanaweza kusababisha hata watu kutoana roho,licha ya kung'oa viti kwa washabiki wa simba. gentleman katabi frm Gongo la mboto
Sheby King 
hizi tv zetu bwana,bado sana jinsi ya kuchukua matukio
Nchimbi Robert 
Ni utovu wa nidhamu na kutojielwa. Hawana uchungu na mali ya umma hata kama vitakarabatiwa hatuwezi kuviita orijinali.
arnold van d.Doreen 
simba wepewe hazabu 2 kwnn wafanye hvy kwny viti vya uwanja wa taifa kisa goli
adinan abdulkheri 
Mohamed Dewji atalipa tuuu
Nuru Damasi 
Dah! Inasikitisha sana, na inaniuma Sana kwanini watu hawaipendi nchi yao? Viongozi ameona vema tuwe tunaangalia mechi tukiwa tumekaa kwenye viti, lkn kuna wapumbavu wanavunja, yani nakosa neno la kuwaita maana hata hilo haliwafai, huko ni kujirudisha nyuma kimaendeleo. Kifupi wamekosa akili ya kujiongeza.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx