test

Alhamisi, 13 Oktoba 2016

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 69 & 70 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


Mtunzi : Eddazaria g.Msulwa

 Ilipoishia
Nilimuuliza victoria baada ya yeye kushindwa kuzungumza kitu kinacho mfanya asimame nje ya mlango wetu, akaanza kuvunja vinja vidole vyake kwa aibu, akamtazama john, ambaye hakuwa amezungumza kitu cha aina yoyote, akamshika john shati lake, kisha akamvuta karibu yake na kumpiga busu la mdomo na kunifanya nibaki nikiwa ninamshangao

“I need you john”(john, ninakuhitaji)

Victoria alizungumza huku akimsukumia john ndani ya chumba, changu, kama simba mwenye njaa victoria akamsukumiza john kitandani na kuanza kumvua shati, lake, kwa aibu ikanilazimu mimi kutoka ndani ya chumba nikawaacha waendelee na mambo yao

Endelea
Nikaelekea moja kwa moja jikoni, nikachukua maji ya kunywa kwenye friji lililopo humu jikoni, kisha nikakaa kwenye kiti kirefu ambacho nacho kipo humu ndani ya chumba.Mawazo yakaanza kurudi upa juu ya mtu aliye mteka mke wangu na kumuua kinyama kwa kumlipua kwa bomu

“nilazima nilipize kisasi kwa yoyote aliye husika katika hili”

Nilijiapiza kimya kimya huku nikiyatazama maji yaliyopo kwenye glasi niliyo ishika mkononi mwangu, nikaitazama saa ya ukutani na kukuta ikionyesha ni saa sita kasoro dakika ishirini, usiku

“hawamalizi na sasa hivi”

Nilizungumza huku nikinyanyuka kwenye kiti na kutoka nje, na kuwakuta walinzi wakizunguka zunguka kaimarisha ulinzi wa jumba hili la baba yangu, sikutaka kuzungumza na mtu wa aina yoyote zaidi ya kubatazama mandhari mazuri yalipomo kwenye eneo hili

“hei”
Nilimuita mlinzi mmoja aliye kuwa anakatiza karibu yangu
“ndio bosi”
Kwa bahati nzuri mlinzi huyu alinijibu kwa kiswahili
“ninaweza pata usafiri muda huu”
“kivipi?”

“nina maanisha ninaweza kupata gari, lolote lenye funguo”
“unataka kwenda wapi usiku huu?”
“kuna sehemu ninahitaji kwenda”
“kwa hapo, ndugu siwezi kukusaidia kwani bosi hajatoa ruhusa ya mtu yoyote kutoka na usafiri, tena muda huu wa usiku”

“ahaa powa asante”

Nikaachana na mlinzi na kurudi ndani, nikafika hadi mlango wa kuingilia chumbani kwangu, nikaweka sikio la upande wa kulia, nikasikia miguno ya mahaba ikiwa inaendelea ndani ya chumba change.
“mmmm kazi kweli kweli”

Nikapata wazo la kwenda chumbani kwa victoria japo kuegesha kichwa change kidogo, hii ni kutokana na uchovu mwingi.Nikaingia na kuwasha taa, kitu cha kwanza nikakutana na mwanga wa simu ya victoria, ikionyesha ni muda mfupi kuna meseji au simu ilipigwa.Nikapiga hatua hadi kitandani ilipo, nikaichukua na kutazama, na kukuta missed call na namba ambayo haikuwa na jina lolote.Nikafungua kipochi chake kilicho kuwa pembezoni mwa simu, nikakuta noti kumi za dola mia mia

“yess, kazi yangu imeanza kukamilika”

Nikazichomoa noti hizo, na kuzidumbukiza kwenye mfuko wa jinzi langu, ambapo kuna simu ya john, aliyo nikabidhi muda wa mchana.

Nikatazama salio kwenye simu ya victoria nikakuta lipo lakutosha, nikaiweka mfukoni, nikafungua kabatini kwake na kukuta makoti mengi makubwa ya baridi.Nikachukua koti jeusi na kulivaa, nikachukua kofia ya kuzuia baridi na kuivaa, nikatoka nje ya chumba cha victoria.Kutokana ni mzoefu sana wa jumba hili la baba haikuwa, ngumu sana kwangu kutoroka pasipo walinzi kunioa, nikatoka nje ya ukuta wa jumba hili, kwa kuuruka, nikaanza kutembea kuelekea barabara kuu, kwa bahati nzuri nikapata taksi

“nipeleke kwenye uwanja wa ndege, wa ‘johannesburg’, itakuwa ni bei gani?”
“dola mia”
“sawa”
Kutokana nina kiasi cha kutosha cha pesa, sikuwa na haja ya kumbembeleza dereva huyu, japo ninatambua amenipiga kizinga, kutokana na ugeni wangu, tukatumia dakika ishirini kufika uwanja wa ndege.

“unaweza kunisubiri?”

“bili shaka”

Nikampa dereva taksi pesa yake, nikaelekea sehemu ya huduma kwa wateja, na kuwakuta dada kadhaa wakiwa wamejipanga wakizungumza na baadhi ya abiria waliopo kwenye eneo hili
“samahani dada”
“bila samahani, nikusaidie nini?”

“juzi usiku, kuamkia jana nilifika hapa na ndege ya shirika la nchini philipines, kuna kitu ninahitaji kukipata kwenye kwenye safari ile”

“kitu gani?”

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx