test

Alhamisi, 20 Oktoba 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 27 & 28


MUANDISHI : EDDAZARIA 
ILIPOISHIA
“Si unataka kuniua? Niue sasa”
Halima alizungumza kwa hasira huku ameyang’ata meno yake, akimtazama Fetty anaye tetemeka kwa hasira kali, iliyo pelekea sura yake kukunjana na kutisha mithili ya chui jike, aliye uliwa watoto wake
akishuhudia.Gafla mlio wa risasi ukasikika huku kishindo kikubwa cha mtu kuanguka chini kikisikika
ndani ya chumba walichomo.

ENDELEA
Wote macho yao wakayapeleka sehemu alipo angukia mtu huyo, aliye pigwa risasi na kukuta ni yule nahodha msaidizi akiwa chini amelala huku, damu zikimtoka kifuani mwake na kwenye mkono wake wakulia akiwa ameshika bastola ikiashiria kwamba alitaka kuwashambulia wote waliomo ndani ya chumba ila Anna alimuwahi.

Halima akatoka na kuwaacha wezake kwenye chumba walichopo, akatoka nje ya manohari na kupanda juu kabisa, akawasha sigara yake taratibu na kuanza kuvuta, huku  akijaribu kuishusha hasira yake iliyo tokana na wezake kumuamini Samson, ambaye hataki hata kumuona kwenye macho yake.
                                                                                           *********
Rahab na raisi Praygod Makuya walipo malizwa kufunguliwa kamba zao kwa ajili ya kudumbukizwa kwenye jungu kubwa lenye maji yaliyo chemshwa kwa ajili yao. Rahab akamkonyeza muheshimiwa raisi na hapo hapo, wakaanza kupambana na vijeba hivyo vipatavyo sita, na kuwafanya watu wengine walio kusanyika katika eneo la uwanja kushuhudia kuuawa kwao, ili wawale wakaanza kuchanganyikiwa kwani kwa mapigo aliyo kuwa akiyapiga Rahab, yalimshangaza hadi chifu wao, hakuamini kuona mtoto wa kike akipambana kwa kiasi cha kuwaangusha vijeba wenye miraba miine.
“Twende muheshimiwa”

Rahab alizungumza baada ya kupata kijinafasi cha kukimbia kutoka kwenye kundi kubwa la watu hawa. Wakaanza kukimbia kuiingia msituni huku wakifwatwa kwa nyuma na kundi la askari wa kijiji hichi ambao wanatumia mishale na upendi katika kuwashumbulia. Kila walivyo kimbia ndivyo kundi la askari hao lilvyo zidi kuwafukuzia, na mbaya zaidi, mwanga wa mbalamwezi ulimulika kila upende wa anga na kuwafanya washinde kujificha kwenye vichaka kuhofia kuonekana na kukamatwa tena.
“Nimechoka…..”

Raisi alizungumza huku akionekana kukatishwa tamaa na kukimbia huko, Rahab akamshika mkono raisi na kuendelea kukimbia, kwa bahati nzuri wakakuta moja ya pango, wakaingia pasipo kuchunguza ndani ya pango hili kutakuwa na kitu gani. Askari hao waliokuwa wanawakimbiza wakapita kwa spidi katika pango hilo pasipo kuchunguza sana kama watu wanao wakimbiza watakuwa wameingia ndani ya pango hilo.
“Asante tena binti”

Rahisi alizungumza huku akiendelea kuhema kwa fujo, akionekana dhahiri kwamba hakuwa ni mtu wa mazoezi. Hawakuwa na sababu ya kuendelea kukaa tena ndani ya pango hilo baada ya kikundi hicho cha askari kupita kwa kasi katika eneo hilo. Wakabadilisha muelekeo na kupita katika njia tofauti na walio kwenda askari hao, ambao laiti wakitiwa mikononi basi hukumu yao ni ile ile ya kwenda kutafunwa nyama. Usiku mzima wakautumia kukimbia, na kutembea pale ilipo walazimu kufanya hivyo, hadi kunapambazuka bado wapo kwenye msitu huu ambao hawaelewi wanaweza kujitoa.
“Tunaweza kupumzika sasa”

Rahab alimuambia muheshimiwa Raisi, baada ya kupata eneo lililo tulia na lina maficho ya wao kupumzika. Raisi Praygod hakuwa na kipingamizi zaidi ya kutafuta sehemu na akajibwaga kama mzigo, miguu yake yote ikawa inawaka moto kwa jinsi alivyo kimbia na kutembea kwa muda mrefu, akavivua viatu vyake na kuviweka pembeni kisha akajilaza.

Rahab akasimama na kuanza kulichunguza eneo zima, kuhakikisha kama wanaweza hata kujilaza kidogo katika sehemu hiyo pasipo buguzi. Akiwa katika kuchunguza chunguza sehemu akabahatika kupata kuona mti wenye matunda mengi makubwa na mazuri, akausogelea na kulichuma tunda moja, akalipasua na kulilamba. Akapata laza tamu ya tunda hilo ambalo hakujua ni tunda la aina gani. Akaanza kulitafuna taratibu kusikilizia kama kuna madhara yoyote atakayo yapata, ila haikuwa hivyo kadri jinsi alivyo zidi kulila ndivyo jinsi alivyo zidi kunogewa na tunda hilo, na wala hakusikia mabadiliko yoyote katika mwili wake. Akachuma mengi kidogo na kurudi sehemu alipo lala muheshimiwa raisi Praygog.

“Muheshimiwa amka”
Rais akajinyanyua kivivu na kukaa kitako, huku akipiga miyayo, akiashiria kwamba yupo katika hali ya uchovu mkubwa. Rahab akampa tunda moja muheshimiwa kwa ajili ya kupunguza njaa ambayo inaendelea kukwangua matumbo yao, muheshimiwa raisi akaanza kula matunda hayo.
“Matunda gani haya?”

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx