Timu ya taifa ya Tanzania ya vijana chini ya umri wa miaka 17 maarufu kama Serengeti Boys iliwasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere usiku wa October 4 2016 ikitokea Congo Brazzaville ilipokwenda kucheza mchezo wake wa maruadiano.
Serengeti Boys waliwasili Dar es Salaam wakitokea Congo Brazzaville
baada ya kucheza mchezo wao wa marudiano wa kuwania kufuzu kwa mataifa
ya Afrika kwa wenye umri chini ya miaka 17 ambayo yatafanyika 2017 Madagascar, baada ya kufungwa goli 1-0.
Vijana hao ambao wametolewa kwa kufungwa magoli mengi nyumbani walienda Congo
wakiwa na ushindi wa goli 3-2, hivyo kufungwa goli 1-0 kunawafanya
watolewe kwa kigezo cha kuruhusu kufungwa magoli mengi nyumbani licha ya
kuwa aggregate inasomeka 3-3.
ALL GOALS YANGA VS SIMBA

