test

Jumamosi, 24 Septemba 2016

Sababu kuu zinazo mkosesha mwanamke hamu ya tendo la ndoa


Tunapozungumzia mwanamke kukosa uwezo wa tendo la kujamiiana hapa tunamaanisha anakuwa hana hamu ya tendo hilo au hata akilifanya hafurahii.

Uwezo wa kufanya tendo la kujamiiana kwa mwanamke tunategemea unapungua taratibu kuanzia umri wa miaka hamsini, siyo unaisha ila unaanza kupungua taratibu kadiri umri unavyosonga mbele hadi baadaye unaisha kabisa.BLACK WOMAN

Katika umri huo ndipo tunategemea kusikia mwanamke anaanza kusema hamu ya tendo hilo inapungua au imepungua na hata akilifanya hafurahii kama zamani, hii inatokana na upungufu wa vichocheo muhimu vya ‘Estrogen’ ambavyo ni lazima vipungue katika umri huo ambao mwanamke tayari ameshafikia ukomo wa hedhi na uzazi. Endapo vichocheo hivi vitaendelea kuwa juu katika umri huo au ataviongeza, basi kuna hatari ya mwanamke kupata saratani ya mfuko wa uzazi.

JINSI TATIZO LINAVYOTOKEA

Hali ya kutohisi hamu ya tendo na kutopata raha ya tendo ni ya kawaida katika umri mkubwa wa mwanamke kuanzia miaka 50 lakini si ya kawaida katika umri wa chini ya hapo, siyo kawaida kwa mwanamke wa umri wa miaka 20 hadi 48 kupata tatizo hili. Endapo mwanamke wa umri huu atalalamika hali hiyo basi ni tatizo linalohitaji uchunguzi wa kina.BLACK COUPLE

Katika umri wa kuzaa, pale mwanamke anapoendelea kupata siku zake kama kawaida tunategemea mwili wake upo vizuri, homoni zake zinafanya kazi vizuri na anafurahia maisha yake.

Kutohisi hamu ya tendo la ndoa ni kutopata hisia za kimapenzi hata akimuona mwenzi wake, akiguswa au hata akiambiwa maneno ya mapenzi hapati hisia wala msisimko wowote wa kimapenzi. Mwanamke asiyefurahia tendo la ndoa ni yule asiyefikia kilele cha tendo hilo, mwanamke akifikia kilele hutoa majimaji na huwa na hali ya kumaliza tendo na kupumzika lakini akiwa na tatizo hili hafikii hapo na hufanya tendo hilo basi tu na humridhisha tu mpenzi wake.

DALILI ZA TATIZO

Mwanamke mwenye tatizo la kutohisi hamu huwa yupo tu na anaweza kukaa muda mrefu hata zaidi ya mwaka bila kufanya tendo hili na hana tatizo lolote, huendelea tu na shughuli zake. Mwenyewe atakuambia labda mwenzake amuanze lakini vinginevyo hajisikii hamu kabisa. Kitaalamu hawezi kupata tatizo lolote kiafya labda kama yupo kwenye uhusiano ndiyo italeta mgogoro. Mwanamke asiyefurahia tendo anaweza kuwa na historia ya kuwa na maumivu wakati wa tendo, kama alishawahi kuingiliwa kwa nguvu au kama mwenzake yaani mume ana matatizo wakati wa tendo aidha hawezi au hamfikishi mara kwa mara.BLACK WOMAN

Kutofurahia tendo kwa muda mrefu humuathiri mwanamke katika afya yake ya akili na hulifanya kwa kujilazimisha. Wanawake wengi wenye tatizo hili chanzo huwa ni wanaume kushindwa kumudu tendo hili.

MATIBABU NA USHAURI

Tatizo hili halina dawa maalumu, jambo la msingi ni kujua chanzo chake na kukitibu. Uchunguzi utazingatia mambo mbalimbali kutegemea na daktari atakavyoona inafaa.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx