test

Jumatatu, 26 Septemba 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 15 & 16



MUANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA 

ILIPOISHIA
“Fanya fasta basi”
Samson akatoka nje huku akiishika shika pua yake iliyo jaa maumivu ya kupigwa ngumi na Rahab, Samson akaingiza baiskeli ya kwanza na kutoka nje akiwa ameishika baiskeli ya pili akitaka kuingia ndani, gafla breki za gari aina ya Defender yenye askari wa kikosi cha F.F.U wapatao sita wakashuka kwenye gari kwa haraka huku wakiwa na bunduki na kunza kumfwata Samson sehemu alipo simama

ENDELEA
“Unafanya nini hapo?”
Askari mmoja alizungumza kwa sauti ya ukali na kumfanya Samson kuanza kutetemeka mwili mzima
“Husikii au?” askari aliendelea kuzungumza kwa sauti ya ukali

“Ni..ninaingiza baiskeli zangu ndani”
“Wewe kama nani?”
“Mimi, ni mmiliki wa hapa, mchana nilikimbia kutokana na tukio la majambazi”
Mazungumzo, yote yanavyo endelea nje Rahab anayasikiliza kwa umakini wa hali ya juu, huku bastola yake ikiwa mkononi mwake
“Mkuu tukague ndani”
Ombi  la askari huyu mwenye alama ya ‘V’ kwenye bega moja, likamfanya Samson kubaki akiwa anaduwaa, ila akajikaza asiuonyeshe mstuko wake kwani hakujua kitatokea nini baada ya askari hao kuingia ndani ya duka lake na kumkuta Rahab
“Kuna vurugu, maeneo ya Sinza kwa Remy, OVER”
Ilisikika sauti kupitia redio ya upepo aliyo ishika mkuu wao na kusababisha, kuto kulijibu ombi la asakri wake
“Tunakuja Over”

Alijibu, huku akiiwatazama askari wake na wote kwa pamoja wakarudi kwa haraka kwenye gari lao na kuondoka kwa kasi kubwa.Sammso akashusha pumzi nyingi, kwa haraka akaanza kuingiza baiskeli zake zote
“Tuondoke, tayari nimesha maliza”
Samson alimuambi Rahab na wote wakatoka nje kwa umakini, huku wakichunguza kila eneo la nje.Samson akapanda kwenye baiskeli yake
“Panda twende”
Rahab akaitazama baiskeli ya Samson kwa umakini,
“Siwezi kukivunja kiti chake”
“Wewe panda twende kwani kikivunjika tutajua mbele ya safari, isije hawa jamaa wakarudi na kunikuta tupo pamoja hapa sijui itakuwaje”
“Mmmm!!”

Rahab akapanda kwenye baiskeli na taratibu Samson akaanza kubadilisha gia moja baada ya nyingine zilizopo kwenye baiskeli yake kutoka gia laini kuelekea gia ngumu, na jinsi anavyozidi kuendesha baiskeli ndivyo mwendo wa baiskeli yake inavyozidi kuongezeka.Ndani ya dakika kumi wakawa wamefika nyumbani kwa Samson, wakaingia ndani kisiri pasipo mtu yoyote kuwaona

Ukimya ukatawala kati yao, na hakuna mtu aliye msemesha mwenzake kwa wakati huu, alicho kifanya Rahab, akavua viatu vyake na kupanda kitandani na kumfanya Samson kuendela kusimama akimtazama Rahab jinsi alivo jilaza chali akitazama paa la chumba chake

“Panda ulale”
Rahab alizungumza huku akimtazama Samson usoni
“Ahaa, mimi nitalala hapa chini”
“Wewe vipi, kinacho kuogopesha wewe ni nini?”
“Siogopi”
“Sasa kinacho kubabaisha ni nini, hebu acha ufala panda kitandani kwako ulale, ila onyo lala usiniguse mwili wangu”
“Mmmmm”
“Guna, tu”
“Ndio maana ninakuambia kwamba nitalala hapa chini”
“Sijawai kuona dume zima likiwa linaogopa kulala na mwanamke kitanda kimoja”

Samson akamtazama Rahab kwa umakini kisha akapanda juu ya kitanda na kuchukua mito miwili na kutengeneza mpaka kati yao ambao hakuna mtu ambeye angeweza kumgusa mwengine, Samson taratibu akajikuta akiaanza kutawaliwa na hisia za mapenzi juu ya Rahab ambaye anaonekana kawa si mtu wa masihara hata kidogo.Samson akauingiza mkono wake mmoja chini ya mto, na taratibu akanza kuupeleka katika eneo alilo lala Rahab.Akafanikiwa kuufikisha mkono wake alipo lala Rahab, akamminya kwenye maeneo ya mbavu , ila Rahab akatulia kimya na kujifanya kama amelala, Samson akarudia tena kumminya Rahab eneo la mbavu na Rahab hakuonyesha mtikisiko wowote

“Kitu kimelinki”
Samson alizungumza kimoyo moyo, huku usoni mwake akiachia tabasamu pana lililojaa uchu mkali wa mapenzi, akajigeuza na kujilaza kiubavu, taratibu mkono wake mmoja ukaanza kupandisha hadi kwenye chuchu ya Rahab, hata kabla Samson hajaukandamiza mkono wake vizuri kwenye chuchu ya Rahab, gafla macho yake yakakutana yakitazamana na jicho la bastola, aliyoishika Rahab kwa umakini

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx