test

Jumanne, 28 Juni 2016

Waziri Lukuvi sasa kumaliza mgogoro wa shamba la Sumaye Mabwepande


Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu wa ardhi katika eneo la Mabwebande Dar es salaam ambao unamhusisha Waziri mkuu wa zamani, Frederick Sumaye na wananchi.

Baaada ya juhudi mbalimbali za kutafuta suluhu ya kudumu, uongozi wa Mkoa wa Dar es salaam na Wilaya ya Kinondoni umemuomba Waziri wa ardhi, William Lukuvi kufika kwa ajili kumaliza mgogoro na kuupatia suluhu ya kudumu.
Eneo la shamba linalomilikiwa na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye linadaiwa kuwa wananchi walilivamia baada ya kuona haliendelezwi kwa muda mrefu na kuweka makazi katika shamba hilo lenye hekari 33. Akizungumza na Ayo TV, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amesema…….
>>>’Mzee Sumaye anamiliki shamba la hekari 33 ambalo halijaendelezwa tangu 1990, jambo ambalo limefanya wananchi zaidi ya 1800 wakiangaika kutafuta makazi katika eneo hilo la shamba
>>>‘Waziri Lukuvi atafika katika eneo la Mwabepande kwa ajili ya kuleta ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro huu ambao tumekuwa tukiushughulikia kwa muda mrefu’

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx