test

Jumanne, 11 Oktoba 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 23 & 24



MWANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
“Tutaonana kuzimu”
Kabla hata Rahab ajafyatua risasi ya aina yoyote ndege ikayumba gafla na kuwaangusha raisi na Rahab, kutokana na Samson kuifunga mitambo yote ya ndege, ikiwemo mashine baadhi za uendeshaji wa ndege, zimesababisha marubani kushindwa kuikwepa ndege ya abiria ya shirika la Fly Emirates, ambayo zimekutana kwenye njia moja, marubani wa ndege ya abiria hawakuweza kuiona mapemba ndege ya Raisi wa Tanzania, kutokana na kushindwa kuiona kwenye rada zao, na wakajikuta wakiingonga, ndege ya raisi wa Tanzania kwenye ubavu wa nyuma wa ndege na kuisababisha kugeuka mara mbili na kuanza kwenda chini kwa kasi sana, huku ndege yao ya abiria ikiianza kuwaka moto

ENDELEA
Kelele za abiria zilizo andamwa na  vilio vya uchungu, ziliendelea kusikika kwenye ndege ya raisi wa Tanzania bwana Ptraygod Makuya, kwajinsi ndege inavyozidi kwenda chini ndivyo jinsi ilivyozidi kuwaka mato mwingi na kuendelea kupasuka baadhi ya sehemu na kuzidi kulete maumivu makali kwa kila abiria aliye kubwa na kitu chochote kikali, ambacho kinaugusa mwili wake na kuzidi kumuumiza, huku wengine wakijikuta wakipoteza viungo vyao vya mwili.Hali hii inaendelea sawaswa na hali iliyopo ndani ya ndege ya abiria iliyo gonga sehemu ya nyuma ya ndege ya Raisi.Ndani ya chumba walichopo Samson, Rahab na rais Praygod, hali inazidi kuwa mbaya, kwani computer zote zinaanza kulipuka moja baada ya nyingine, kwa haraka Rahab anajitahidi kushikilia moja ya nguzo ya chuma, huku mkono wake mmoja akimshikilia Raisi ambaya anavutwa na upepo mwingi, unaoingia kwenye chumba chao, ukitokea nje kutokana na ukuta wa chumba chao kutoboka kutokana na motom mkali  unaoendelea kuiteketeza ndege

“Muheshimiwa Raisi endelea kujikaza”

Rahab alizungumza kwa sauti ya juu huku mkono wake wa kulia, akiendelea kumshikilia Raisi, huku mkono wake wa kushoto pamoja na mguu wake wa kulia kwa pamoja vikiwa vimezunguka kwenye nguzo ya chuma inayo endelea kumsaidia asitoke nje ya chumba hicho.Hali kwa upande wa Samson inazidi kuwa ngumu sana kutokana na upepo mwingi kuendelea kuingia ndani ya ndege, kutokana na kipigo kikali alicho kipata kutoka kwa Rahab, ambacho kimempelekea mikono yake kukosa nguvu ya kushikilia kwenye baadhi ya vitu vilivyomo ndani ya ndege.Samson anajikuta akiachia kwenye moja ya sehemu aliyo ishikilia na upepo mkali unamtoa nje, huku akipiga kelele za kuomba msaada, Ndege nayo ikazidi kwenda chini kwa kasi kubwa huku, ikizidi kuchanguka baadhi ya maeneo yake
                                                                                                 ***
Baada ya Fetty kukata simu anawageukia manahodha wawili wanao kiendesha chombo cha kivita kijulikanacho kwa jina la ‘Sabmarine’ au Nyambizi, huku mkononi mwake akiwa ameishika bunduki yake aliyopiga risasi kadhaa pembeni

“Mutafanya kile ambacho mimi nitawaelekeza, Sawa?”

Fetty alizungumza huku bunduki yake akiwa ameielekeza kwa wanahodha hawa, ambao nao ni wanajeshi wa wajeshi la maji nchini Tanzania,

“Sa…wa”
Mmoja alijibu huku mwili wake ukimtetemeka sana, hadi haja ndogo akaanza kuihisi ikimwagika

“Kwanza hapa tulipo ni wapi?”
Anna aliuliza kwa sauti ya ukali
“Hapa tupo bahari ya Pasifiki maharibi kwa bara la Asia, katika nchi ya Australia”

Nahodha mmoja alizungumza huku akitazama kifaa maalumu ambacho kina namba nyingi, ambazo kwa mtu wa kawaida si rahisi kuweza kugundua ni nini kinacho tazwamwa

“Mmmmmmm…..!!”
Halima aliguna huku akiwatazama wezake kwani hakuelewa kitu kinacho zungumzwa hapo ni kitu cha aina gani
“Tutarudi vipi Tanzania?” Agnes aliiuliza
“Tanzania tumeiacha mbali sana?”
“Ndio tutarudi vipi Tanzania” Fetty aliuliza kwa sauti ya ukali, na kuwafanya manahodha kuzidi kutetemeka
“Tutar….”

Kabla nahodha mmoja ajamalizia sentesi yake, akastushwa na kingora kilichopo pembezoni mwa chumba chao kikianza kulia huku kifaa kingine mbele yao chenye kioo kikukubwa mithili ya simu aina za I pad, kikianza kuonyesha vitu vilili virefu vyenye rangi nyekundu vikija kwa kasi sana

“Mungu wangu, ni mabomu haya”

Nahodha mmoja ambaye umri wake umekwenda kidogo alihamaki huku kajasho kakianza kumwagika usoni mwake akitazama kioo hicho kwa macho yake makubwa kiasi

“Mabonu……!!?”
Anna aliuliza huku naye macho yakiwa yanamemtoka
“Ndio, tumeshakamtwa kwenye rada ya  nchi ya Australia”

Kila mmoja akaanza kuomba sala yake ya mwisho, kutokana na mabomu hayo kuzidi kuja kwa mwendo wa kasi huku yakionekana kukilenga chombo chao ambacho kinapita kwa siri chini ya bahari hii kubwa ya Pasific, katika eneo la jeshi la nchini Australia

==>Endelea  Nayo  <<Kwa  Kubofya  Hapa>>

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx