Skip to content
Kampuni
ya uchimbaji wa madini ya Acacia kupitia Mgodi wake wa Buzwagi
umekabidhi madawati 4494 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 548
kwa ajili ya shule za sekondari na msingi za mkoa wa Shinyanga.
Akikabidhi madawati hayo,meneja mkuu wa
mgodi wa Buzwagi Mhandisi Asa Mwaipopo amesema Kampuni yake imekabidhi
kiasi hicho cha madawati kwa lengo la kuunga mkono jitihada za
mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Dkt. John Pombe
Magufuli kupunguza uhaba wa madawati katika shule za msingi na
sekondari.
“Mgodi wa Buzwagi unaunga mkono
jitihada zinazofanywa na rais wa awamu ya tano,Dkt. John Pombe Magufuli
katika kumaliza tatizo la wanafunzi kukaa chini,tumeamua kutekeleza kwa
vitendo jitihada hizo” ,alieleza Mwaipopo.
Akipokea madawati hayo Mkuu wa mkoa wa
Shinyanga, Bi Zainab Telack ameupongeza mgodi wa Buzwagi kwa mchango wao
uliolenga kuunga mkono jitihada za mheshimiwa rais Magufuli, katika
kuhakikisha kuwa watoto wote wanakaa kwenye madawati.
“Nimefarijika sana kuona mnaunga
mkono serikali,tulikuwa na upungufu wa madawati lakini kwa msaada huu wa
madawati mmesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo”,alisema Telack.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa wa Shinyanga
amewataka wakurugenzi wa halmashauri zote katika mkoa wa Shinyanga
kuwachukulia hatua kali za kisheria wazazi wote wanaowaachisha masomo
wanafunzi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
Halmashauri ya mji wa Kahama Abeli Shija akishukuru kwa niaba ya
halmashauri za mkoa wa Shinyanga, ameupongeza Mgodi wa Buzwagi kwa
jitihada zao mbalimbali katika kutekeleza miradi ya kimaendeleo katika
mkoa wa Shinyanga na hususani wilaya ya Kahama.
Hafla hiyo ya kukabidhi madawati
ilifanyika Julai 28,2016 katika Shule ya Msingi Majengo iliyoko wilayani
Kahama katika halmashauri ya mji wa Kahama ambapo ilihudhuriwa pia na
wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga,viongozi wa
wilaya ya Kahama,uongozi wa Mgodi wa Buzwagi, walimu na wanafunzi wa
shule ya msingi Majengo.
Meneja
mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Asa Mwaipopo(mwenye kofia ya bluu) akimpokea
mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack wakati wa hafla ya kukabidhi
madawati 4494 yaliyotolewa na Mgodi wa Buzwagi unaomilikiwa na Kampuni
ya uchimbaji wa madini ya ACACIA.
Wanafunzi wa shule ya msingi Majengo
iliyopo katika halmashauri ya mji wa Kahama wakipiga makofi kumkaribisha
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga wakati wa hafla ya kupokea madawati kutoka
kwa uongozi wa Mgodi wa Buzwagi.
Wanafunzi
wa shule ya msingi Majengo moja ya shule zilizonufaika na mchango wa
madawati yaliyotolewa na Mgodi wa dhahabu wa Buzwagi.
Meneja
Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Mhandisi Asa Mwaipopo na Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga Bi Zainab Telack wakifurahia jambo muda mfupi kabla ya
makabidhiano.
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama Simon Berege akizungumza
wakati wa hafla ya kukabidhi madawati kutoka kwa Mgodi wa Buzwagi.
Meneja
mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Mhandisi Asa Mwaipopo (kushoto) akiteta jambo
na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Zainab Telack wakati wa hafla ya kukabidhi
madawati kwa uongozi wa mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Abel Shija akizungumza na kuushukuru
Uongozi wa Mgodi wa Buzwagi unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia kwa msaada
wa madawati ambayo halmashauri ya mji wa Kahama itanufaika nayo.
Mhandisi
Asa Mwaipopo Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi akizungumza wakati wa
kukabidhi madawati yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 548 kwa
mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Wanafunzi wakifuatilia hotuba ya meneja mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Mhandisi Asa Mwaipopo
Mkuu
wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zainab Telack akikata utepe kuashiria kupokea
madawati 4494 kutoka kwa uongozi wa Mgodi wa Buzwagi, anaekabidhi ni
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Mhandisi Asa Mwaipopo.
Mkuu
wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zainab Telack (katikati) akiwa amekaa na
wanafunzi wa shule ya msingi majengo wakati wa hafla ya kupokea madawati
kutoka kwa mgodi wa Buzwagi.
Mkuu
wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zainab Telack (kulia) akiwa amekaa kwenye
dawati na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Mhandisi Asa Mwaipopo.
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Msalala Simon Berege akifurahia kukalia moja ya
madawati yaliyokabidhiwa na Mgodi wa Buzwagi kwa Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zainab Telack akihutubia baada ya kupokea madawati 4494 kutoka Mgodi wa Buzwagi
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Shinyanga na wilaya ya Kahama wakiwa katika hafla hiyo.
Mkuu
wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkulu(katikati) akiteta jambo na katibu
tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela (kulia), mwingine katika
picha ni mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama, Anderson Msumba
(Kushoto).
Meneja
mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Mhandisi Asa Mwaipopo (Katikati) akiagana na
Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Kahama Bwana Abel Shija, wengine
katika picha kutoka kushoto kabisa ni Moses Msofe Mkuu wa Kitengo cha
Mahusiano ya Jamii, Mhandisi Richard Ojendo (wa pili kutoka kushoto)
Mshauri wa Miradi Kampuni ya Acacia.
Wanafunzi wa shule ya Msingi Majengo
wakifurahia mara baada ya shule yao kupokea baadhi ya madawati kutoka
kwa uongozi wa Mgodi wa Buzwagi.
Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi
xxxxxxxxxxxxx