test

Alhamisi, 12 Aprili 2018

Mashabiki wa Yanga wavamia makao makuu ya Klabu usiku kumsaka Mkwasa,sababu ni Lwandamina




Baadhi ya mashabiki na wanachama wa Yanga walivamia ofisi za Makao Makuu ya klabu jana usiku  wakimtaka Katibu Mkuu, Charles Boniface Mkwasa.
Mashabiki walijiitokeza Makao Makuu ya klabu wakimtamka Mkwasa awape ufafanuzi kuhusiana na kuondoka kwa Kocha George Lwandamina ambaye amerejea kwa Zambia kujiunga na timu yake ya zamani, Zesco United.

Baada ya kuwasili ofisini hapo, wengi wameonekana wakimtupia lawama Mkwasa, wakisema kuwa yeye ndiye chanzo cha kuondoka kwa Lwandamina kimyakimya.
Taarifa zilizoripotiwa baada ya kuondoka kwa Lwandamina, zinaeleza kuwa Mkwasa na Kocha huyo hawakuwa na maelewano mazuri haswa katika masuala mazima ya utendaji.
Mbali na utendaji, inaelezwa pia Mkwasa ana mpango wa kuachana na wadhifa wa Ukatibu Mkuu ili kuchukua nafasi ya Lwandamina.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx

0 comments:

Chapisha Maoni