test

Jumatano, 16 Novemba 2016

Mwigulu Afanya Ziara Makao Makuu Uhamiaji.......Aagiza Wahamiaji Haramu Warudishwe Nchini Kwao


Serikali imeagiza idara ya uhamiaji nchini kufanya uhakiki upya wa vibali vya wahamiaji wote walioko nchini na kwa wale ambao hawana sifa zinazostahili warudishwe kwenye nchi zao kwakuwa wanaishi nchini kinyume na sheria za nchi zinavyoelekeza.

Agizo hilo limetolewa jana na waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhe. Mwigulu Nchemba alipokutana na viongozi wa idara ya uhamiaji nchini kwaajili ya kujadili na kutatua kero mbalimbali katika idara hiyo.

Kwa upande wa mifumo ya utoaji vibali Mhe. Mwigulu ameiagiza idara hiyo iunde tume maalum ya kujadili nakuangalia namna ya kuweka mifumo maalum ya kutoa vibali vya uraia kwa urahisi ili kupunguza malalamiko na ufisadi ambao kama hautatatuliwa mapema utasababisha hasara kwa taifa.

Aidha aliwaagiza watawala katika idara hiyo kutenda haki kwa watumishi wake na watanzania kwa ujumla sambamba na kuwalipa madeni yao watumishi wapya walioajiriwa na idara ya uamiaji nchini.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx