test

Jumanne, 6 Septemba 2016

Bandari ya Dar yapaisha mapato TRA


SIKU moja baada ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, kueleza kushitushwa na kupungua kwa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam, Mamlaka ya Mapato (TRA) imeeleza kuwa makusanyo ya kodi katika bandari hiyo, yanaongezeka kwa kasi.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Richard Kayombo akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake leo.(Picha na Mroki Mroki). 
Ongezeko la makusanyo katika Bandari ya Dar es Salaam ni sehemu ya makusanyo ya kodi, yaliyowezesha TRA kuweza kukusanya Sh trilioni 1.158 katika makusanyo ya mwezi Agosti mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi TRA, Richard Kayombo alisema kuwa mapato hayo ni kutokana na makusanyo kutoka maeneo yote ya kodi. Katika kile kinachodhihirisha kuwa makusanyo katika Bandari ya Dar es Salaam yameongezeka licha ya kuwepo kwa propaganda nyingi kuwa upungufu wa mizigo bandarini umeshusha kodi za serikali,

Kayombo alisema; “licha ya mizigo kupungua bandari ya Dar es Salaam lakini makusanyo ya kodi katika bandari hiyo yameongezeka mara dufu.”

Kayombo alisema TRA imefanikiwa kukusanya kiasi cha Sh trilioni 1.158 katika makusanyo ya mwezi Agosti mwaka huu na kusema kuwa makusanyo hayo yanatokana na mikakati madhubuti waliyojiwekea.

Install Application ya JUNGUKUULEO Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi

xxxxxxxxxxxxx